top of page

Msaada wa Moja kwa Moja

FADHILI MTOTO NA/AU DARASA

Kusaidia Mtoto:
 Kwa kuunga mkono mtoto, unaunda uhusiano maalum kati yako, mtoto anayeohitaji msaada, na jamii ambapo wataalamu wa Children-for-Life wanatekeleza jitihada za kubadilisha mustakabali wa watoto. Kwa Dola za Kimarekani 20 ($20) tu kwa mwezi, unaweza kutoa chakula chenye lishe, vifaa muhimu vya kielimu, na kulipia ada za shule, ili kuboresha ustawi wa mtoto. Hii pia inakupa fursa ya kushuhudia mabadiliko chanya katika maisha ya watoto.

Kusaidia Darasa:
 Kwa kuunga mkono darasa, unaweza kuhakikisha ukuaji wa pamoja wa watoto wanaohitaji msaada na kukuza maendeleo ya jamii kwa pamoja. Kwa Dola za Kimarekani 600 ($600) tu kwa mwezi kwa darasa lenye wanafunzi 30, unaweza kutoa msaada muhimu wa kielimu na lishe, na hivyo kuboresha ustawi wa watoto. Aidha, hii inakupa fursa ya kushuhudia mabadiliko chanya katika maisha ya watoto kwa mustakabali.

Baada ya Kusaini Mkataba wa Ufadhili, yafuatayo yatatolewa:

  • Jina la mtoto/watoto waliopo katika mpango wa ufadhili.

  • Umri wa mtoto/watoto.

  • Jina la shule.

  • Jina la mwalimu anayesimamia.

  • Taarifa za mawasiliano (barua pepe, anuani ya makazi, namba ya simu ya familia/mama wa mtoto/watoto).

  • Ripoti ya maendeleo itatolewa kila robo mwaka, muhula, au kwa ombi maalum.

Tupigie:​​

+255-763-205-703 or

+255-752-699-815

​Pata Ofisi Yetu: 

9 Dagoni Street, Mbweni JKT, Kinondoni District, Dar Es Salaam, Tanzania

Email: info@Childrenforlife.com

© 2015 na Children for Life 

© Copyright
bottom of page